Jumanne 19 Mei 2026 - 07:00
Kurejea kwa Marekani katika zama za utumwa

Hawza/ maelfu ya wanaharakati wa kiraia walipinga kupunguzwa kwa haki za kupiga kura za watu weusi na mabadiliko ya mipaka ya maeneo ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, maelfu ya wanaharakati wa haki za kiraia, viongozi wa watu weusi na waandamanaji wa Marekani walifanya mkusanyiko mkubwa katika mji wa Montgomery, mji mkuu wa jimbo la Alabama, ili kupinga kupunguzwa kwa haki za kupiga kura za watu weusi na mabadiliko ya maeneo ya uchaguzi.

Mkusanyiko huu ulifanyika baada ya uamuzi wa hivi karibuni wa Mahakama Kuu ya Marekani kudhoofisha baadhi ya ulinzi muhimu wa Sheria ya Haki za Kupiga Kura; hatua ambayo kwa mujibu wa wakosoaji imefungua njia ya kupunguza ushawishi wa kisiasa wa wapiga kura weusi.

Waandamanaji walizilaumu serikali za majimbo zinazodhibitiwa na chama cha Republican kwamba kwa kuchora upya ramani za uchaguzi, zinajaribu kupunguza nguvu ya kura ya jamii ya watu weusi kabla ya uchaguzi ujao.

Maandamano hayo yalianzia mji wa kihistoria wa Selma, eneo la tukio maarufu la “Jumapili ya Umwagaji Damu” mwaka 1965, na kuendelea hadi katika jengo la Bunge la jimbo la Alabama.

Cory Booker, seneta wa chama cha Democratic wa Marekani aliyeshiriki katika mkusanyiko huo alisema: “Montgomery ni ardhi takatifu ya harakati za haki za kiraia na hatutaruhusu nchi kurejea katika zama za Jim Crow.”

Wanaharakati wa haki za kiraia wanasema kwamba; mabadiliko mapya katika maeneo ya uchaguzi ni jaribio la kudhoofisha sauti ya watu weusi wa Marekani na kurejesha hatua kwa hatua sera za ubaguzi wa rangi; suala ambalo baada ya hukumu za hivi karibuni za Mahakama Kuu ya Marekani limeongeza wasi wasi mkubwa kuhusu jambo hilo.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha